Kuanzia tarehe 1 Julai mwaka huu mashindano ya kombe la dunia la soka kwa vijana walio na umri chini ya miaka 20yatakuwa yanafanyika. Mwaka huu mashindano hayo yanafanyikia hapa Canada na Toronto ukiwa ndio mji utakaokuwa na mchezo wa kufungua mashindano na pia kufungia(fainali). Afrika inawakilishwa na timu nne ambazo ni Zambia, Congo, Gambia na Nigeria.Jumla ya timu zinazoshiriki ni 24.
Kwa vyovyote vile mashindano haya hayana ushabiki kama yale ya kombe la dunia la wakubwa yaliyofanyika Ujerumani mwaka jana. Lakini kwa washabiki wa soka hapa Canada hii ni nafasi muhimu na ya kipekee katika kujaribu kuukuza mchezo wa soka ambao hauna umaarufu sana hapa ingawa jumuia ya mataifa ya Ulaya na Amerika ya kusini, walio wanazi wa kutupwa wa soka yamejaa hapa. Kuna jumuia kubwa sana wa wareno,wabrazili,wanigeria,waghana,wamexico,waargentina na watu wa kila aina. Inasemekana ni kwa sababu hakuna anayeweka pesa zake kwenye soka.Tusubiri tuone itakuwaje baada ya mashindano haya na pia David Beckham kuhamia huku ambapo atacheza katika ligi ya Marekani (MLS) ambayo Toronto FC wanashiriki pia. Mchezo wake wa kwanza hapa Marekani ya kaskazini unatarajiwa kuwa hapa Canada timu yake mpya ya Los Angeles Galaxy itakapopambana na Toronto FC.
Bwana mdogo Freddy Adu,mzaliwa wa huko Tema nchini Ghana ambaye sasa ni raia wa Marekani ndio anatarajiwa kuwa kivutio kikubwa cha mashindano hayo.Yeye ndio kapteni wa timu ya USA.
Pichani juu ni uwanja wa BMO Field uliopo Exhibition Place.Uwanja huu ndio utakaokuwa na mechi ya ufunguzi na fainali.Unauwezo wa kuwaweka vitini mashabiki 20,000.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 8:37 PM | Permalink |
Huko nasikia mambo ni Aisi Hoki tu!Nasikia ndio mchezo unaolipa kuliko yote ukiwa huko kama mchezaji.Je , na wahamiaji wako sambamba na wenyeji katika mchezo huo?
Halo Jeff, Sijakusoma siku nyingi,hili soka la vijana sisi wabongo hatuna hata timu za vijana. Vilabu vyetu ni sehemu ya majungu tu,na kutafuta kula ya viongozi. Naomba Beckam atakapocheza huko kwa mara ya kwanza utujuze huku.
Huko nasikia mambo ni Aisi Hoki tu!Nasikia ndio mchezo unaolipa kuliko yote ukiwa huko kama mchezaji.Je , na wahamiaji wako sambamba na wenyeji katika mchezo huo?