
Ukiambiwa uzitaje nchi ambazo zimejaliwa kuwa na mandhari nyingi tofauti na za aina yake usisite kuitaja nchi yetu ya Tanzania. Kama kuna mtu anabisha anyoshe kidole. Pichani ni mawe yaliyoko pembezoni mwa Ziwa Victoria jijini Mwanza. Hivi tukilisukuma lile jiwe pale juu litaanguka? Picha kwa hisani ya Ebby Mkandara, mkazi wa hapa Toronto aliyetembelea kanda hiyo ya ziwa hivi karibuni.
Jeff!
aisee hii ni bonge la picha. mpe hongera ebby. basi hapo ingenogab kungekuwa na ndama mweupe akila majani kwa pembeni, ama mbuzi akinywa maji kuleta uhai. lakini bado hiyo peke yake ni postikadi