Siku zote tunajua kwamba nchi yetu inatafunwa na wachache wanaojiita "wajanja".Wengi wetu hatuwezi kusema kwamba eti hatujui wakati kila dalili zipo wazi na wanaoitafuna hujitapa hata wakiwa baa, wakiwa kwenye simu za viganjani hata kwenye daladala.Wanaokula nao wanataka pia kuonekana na wao ni watu wa daraja fulani.Kwa hawa nao tambo ni zile zile...Chukua Chako Mapema.
Tunachokuwa hatukijui na ambacho vyombo vyetu vya habari vinakuwa "bubu" kutuambia ni jinsi gani nchi inaliwa na nani hasa anahusika,akitumia vipi madaraka yake. Hakuna jambo zuri kama kumjua adui yako,silaha alizonazo,mafunzo aliyonayo, mbinu anazozitumia nk.Hawa ndio wale wanaotaka tuamini kwamba "tupo pamoja" na kwamba umasikini wa nchi yetu ni "mipango ya mungu" na hakuna tunaloweza kulifanya. Mipango ya mungu haina makosa!
Mwandishi mmoja wa gazeti la ThisDay katika toleo lake la leo Alhamisi tarehe 24,2007 ameonyesha njia inayoweza kutumika katika 'kuwatambua". Pengine umeshamsoma kwani habari hii imetapakaa kote mtandaoni hivi leo.Nilichotaka kusema ni kwamba nimependa uandishi huu.Tuendelee,tutawajua.
Jeff, nimeshindwa kuipata hii habari. Kiungo kinaponipeleka siioni habari yenyewe. Msaada kidogo. Nataka kuisoma.