Pichani ni basi lijulikanalo kama Executive linalofanya safari zake kati ya majiji ya Dar-es-salaam na Mwanza. Hapo lilikuwa limeharibika.Ndio maana unashauriwa kwamba ukitaka kusafiri ni lazima ujiandae huku ukikumbuka kwamba msafiri kafiri. Picha na Ebby Mkandara, mkazi mwenyeji wa Toronto, aliyekuwa mmojawapo wa abiria walioonja joto ya jiwe na raha za aina zake za Bongo hivi karibuni.Hapo ilikuwa ni Singida. Nasikia ukitaka kufika kaskazini mwa Tanzania vizuri ni vyema ukachukua njia ya kupitia Kenya. Hivi ni kwanini?Kodi zinafanya kazi gani?Suti na safari?
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 5:46 PM | Permalink |
Picha nzuri sana hii!