Tarehe: 7:57:00 AM, Mtoa Maoni:- Simon Kitururu
Tarehe: 7:20:00 AM, Mtoa Maoni:- mwandani
hivi karibuni katika televisheni ya hapa wamekuwa wakionyesha programu "Cuba in Africa odyssey" Hawa jamaa akina Che walikuwa watu wenye moyo wa kimapinduzi sana. ila walishindwa kuwasaidia Wakongo vile akina Kabila walikuwa hawana ufundi wala mikakati - ilibidi waanze kuwafundisha kulenga shabaa - badala ya kuwasaidia kupigana. Halafu double agent wa Kikongo akaenda kuwatonya akina Mobutu na CIA kwamba "Tatu" au Che yuko pahala gani...
Nadhani hasahauliki kwa vile alikuwa ndani ya wakati ambao historia ya dunia ya sasa katika vita baridi ndio ilikuwa ikitengenezwa. Alikuwa mmoja wa wahusika wakuu wa historia hiyo... ambayo ilionyesha nia ya Serikali ya Wamarekani dhidi ya mataifa mengine yanayotaka kujiamulia mustakabali bila kuingiliwa na mabeberu.
Kwa upande wa Afrika hatuwezi kumsahau pia. yeye pamoja na wenzake walikuwa na moyo wa ukombozi.
Hata baada ya kumaliza kusaidia ukombozi Afrika walipoondoka Angola wakati Namibia inapata uhuru, hawakuchukua hata senti tano ya mafuta Angola - walibeba maiti za wapiganaji wao tu!
Huyu jamaa kweli amngekua anafanya hivi kipindi hiki , angeitwa terrorist. Pia angeweza kushtakiwa kama muuaji katika nchi fulani au hata katika Mahakama za kimataifa.