Sikuwa kimya kwa sababu mbaya.Nilikuwa natafakari niseme nini. Msiba wa mbunge kijana Amina Chifupa uliniacha nisijue la kufanya wala kusema. Nilishtushwa kama mlivyoshtushwa watanzania wenzangu. Najua kuna ambao hawakushtuka.Hawa waliuona msiba ukikaribia kwa kuangalia jinsi gani ambavyo historia ya nchi yetu imekuwa tangu enzi na enzi. Kwanini unafunga macho sasa?Kwani wewe hujui kwamba Tanzania hutakiwi kuwasemea walio juu? Kwani hujawahi kuona uozo mbalimbali ukifumbiwa macho kwa sababu waliouona wanaogopa kupoteza maisha yao? Au unataka kujifanya hujui yaliyowahi kutokea siku za nyuma? Acha bwana wewe!
Yawezekana kabisa kifo cha Amina kikawa ni mipango ya mungu. Kinachotia hofu na hivyo kuhalalisha gumzo ni mazingira ya kifo chake. Akasema atawataja hadharani wanaohusika na biashara ya madawa ya kulevya. Magazeti uchwara yakaandika vichwa vya habari na wala yasimuunge mkono wala kuchimba kwa undani.Wakapewa lead lakini wakagwaya.Halafu unataka kunifunga mdomo,Thubutu! Kilichofuata mumewe (ambaye kila afunguaye mdomo anasema yeye pia ni “zungu la unga”) akamtaliki! Sababu aliyoitoa; ugoni! Amina akashindwa kutokea mbele ya waandishi wa habari kama alivyokuwa afanye.Baba mtu akatokea badala yake bila majina ya wazungu wa unga.Akawapa story waheshimiwa waandishi na wao wakakubali. Historia ya Amina ikawa ndio imefikia kikomo.Mauti yakamfika siku ya kuadhimisha vita dhidi ya matumizi ya kulevya!
Kuna vitu vinavyoitwa na wenzetu conspiracy theories.Sijawahi katika siku za hivi karibuni kukutana na nzito zaidi ya hii.Eti nini? Kafariki kwa ugonjwa wa kisukari? Eti alipata ukichaa? Eti malaria? Ipi kati ya hizi sababu inakuingia akilini? Unajua serikali imesema nini? Itafanya uchunguzi wa kifo chake kama itaombwa! Mazingira gani inahitaji? Anewei, ngoja niachie hapa au unataka niseme nini tena?
Kama wewe una anuani ya barua pepe inawezekana kabisa uliupata waraka ulioweka hadharani mambo ya BoT..hujakosea ni ile Benki Kuu ya Nchi! Bila shaka pia ulipata nafasi ya kusoma skandali nzima ya jinsi mihela inavyoliwa na wanaojiita wajanja,wengi wao sio hata raia wa Tanzania. Wabunge wa upinzani ambao ni wachache sana wakaiweka ishu hadharani.Wale wa chama tawala walikuwa wameipata barua pepe lakini wasithubutu kusema. Ngoma ikaenda mheshimiwa mwenye mvi akasema serikali inachunguza. Hapo ndipo niliporuka toka kwenye kiti,almanusura nivunje mguu.Utachunguza vipi wakati watuhumiwa wakuu tukianza na gavana Balali bado wapo ndani ya nyumba? Hivi inaingia akilini kweli? Kwanini katiba ya nchi au aliyemchagua gavana asimwambie mzee kaa kushoto kwanza mpaka uchunguzi uishe? Nani anasoma maandiko haya? Kama hujaisoma dossier ninayoiongelea hapa niandikie e-mail nami nitakutumia.Nchi hii ikoje lakini?
Jeff,
Mambo yenyewe ndiyo kama haya hapa chini:
Government shuns debate on Mkapa
2007-07-04 09:22:47
By Lusekelo Philemon, Dodoma
The government has insisted that it will never work on media reports over allegations leveled against former President Benjamin Mkapa on his involvement in private business while working at the State House.
The government position was stated yesterday by the Minister of State in the President`s Office (Good Governance), Philip Marmo, when debating budget estimates of the Public Service Management.
Responding to requests of the opposition that the government comments on the scandal, Marmo said the government would never work on newspapers reports.
`We will not work on newspapers reports. If there is any one who wants to find the truth of the matter, the procedures are there. The stand of the government is that we will not at any time get involved in such kind of debate. The existing rules and regulations are adequate,` he said.
`The law provides proper channels for any one who is not satisfied with the trend of any leader in this country. Anyone can use those channels by paying only 1,000/- to the ethics tribunal.` Marmo said.
He further explained that the government had circulated about 6, 415 forms to be filled by top government officials to show the property they owned and where and how they got it.
Marmo said there were about 3, 317 government officials who had returned their filled in forms.
* SOURCE: Guardian