Alipojitokeza mbele ya umati wa vyombo vya habari hivi karibuni kuwapigisha story waandishi,gavana wa benki kuu Tanzania,Daudi Balali,alikuwa amejawa na tabasamu.Kwanini asiwe na tabasamu?Kwanza aliruhusu vyombo vya habari alivyovitaka yeye,pili kwa jinsi mambo yanavyokwenda alishajua au anajua nini kitatokea,hata siku laki moja zijazo.Anajua hili litapita,kama yalivyowahi kupita mengine mazito.
Baada ya kusoma kwenye vyombo vya habari yaliyojiri kwenye press conference ile,nilijisemea moyoni mwangu,yametimia. Nisemeje tena? Ulishawahi kusikia serikali yetu ikasikiliza?
Pamoja na hayo,Ansbert Ngurumo amenisaidia kuulinda moyo wangu uliokuwa unakaribia kupasuka kwa kihoro na hasira. Ngurumo amefanya majumuisho ya mengi niliyokuwa nayawaza na kuwazua. Msome hapa.
Hawa jamaa si walishatutangazia kuwa hawasikilizi wala kujadili yaliyoko magazetini?Lakini alichoandika Ansbert wakikipuuzia , ipo siku watastukia wanadakwa tu.Sasa hivi wanalindana na wanajua hakuna litakalo wapata.Lakini kuna leo na kesho