Tarehe: 4:59:00 PM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 10:16:00 AM, Mtoa Maoni:- Bob Sankofa
Huku ndiko hasa tunakokwenda, tunakwenda mahala ambako Mtanzania anaanza kuona kwamba rangi nyekundu ni nyekundu japo viongozi wake wanamlazimisha kusema ni buluu. Miaka ya nyuma Mtanzania wa kawaida alikuwa akisema kuwa nyekundu ni buluu lakini amechoka sasa. Ipo siku Mtanzania atasema "Ahhhhhhhhhhhh!" na ndipo hapo walafi wale watakapokiona cha mtemakuni.
UHURU
Tarehe: 12:43:00 AM, Mtoa Maoni:- mloyi
Sioni tatizo lilikuwa wapi.
Mengi yanasemwa, lakini mimi si mtaalamu wa kiswahili kuweza kuyatofautisha, wansema Zitto kamwambia Mheshimiwa raisi kuwa ni mwongo, alitakiwa atumie neno jingine, kama lipi litakalomaanisha siyo muongo? labda He is just a liar au inawezekana kasema ukweli lakini mimi siamini! inawezekana angemaanisha kitu kilekile! tuwaachie wataalamu wa kiswahili.
Cha kushangaza mbunge akileta hoja ambayo kwa uhakika amepewa na mabosi wake "wapigakura wake" akaomba iundwe kamati ya kuchunguza na yeye anaambiwa athibitishe hizo tuhuma sijui maana yake huwa ni nini? Sasa yeye akithibitisha hizo tuhuma kazi ya hiyo tume itakuwa ni nini? Kama angekuwa na uthibitisho angeomba tume ya nini?
Tuangalie bunge letu linapotupeleka, walianza na bajeti yenye kutuumiza wakaisifia sana kwa kutumia "utapeli wa kishairi" sasa wanawazima wenye hoja zenye maslahi ya kitaifa kwa kutumia nguvu na Mashairi ya kitapeli.
Vilevile nashindwa kujua Spika alitumia kigezo gani kusema waliokubaliana na adhabu ya Zitto walikuwa wengi, Najua kuna watu wanaweza kusema maneno hata matano kwa wakati mmoja hivyo pengine watu walikuwa wanasema ndiyo mara nnenne pale. Nadhani lile Kundi (bunge) ni kundi la watu wasimakini kwenye maamuzi yao.
Tarehe: 8:08:00 AM, Mtoa Maoni:- Ansbert Ngurumo
Tarehe: 9:46:00 PM, Mtoa Maoni:-
Kwa kweli serikali yote ya Tanzania ni ya thugs tu tena very ignorant. Wewe kama mtu akubaliani na wewe unamfukuza bungeni, kama wewe sio ignorant wa mwisho. Mimi sioni hata kama ni ubabe spika aliutumia, ni ku-kiss ass ya Kikwete na woga tu kwamba Zitto anasema ya kweli.
Sijui hawa viongozi wa Tz wanafikiria watanzania wote ni wajinga wasiojua kusoma wala kuandika ndio maana wanajiendeshea mambo kama serikali ni familia yao binafsi, hawafikirii kitu kingine chochote kile. Yaani inasikitisha sana kwa kweli kuona mambo kama haya yanatokea Tz. Wajiangalie sana hao wazungu wanaowauzia nchi kidogokidogo,Tz hawatawapa hata pa kula.
Watatoa onyo mpaka nani hii arudi mara ya pili. Uhuru wa kujieleza wasidhani tutauachia eti kutokana na kuonywa. Katiba inaturuhuru na katiba ndio tunayoitazama na sio onyo toka kwa wezi wa demokrasia. Wanafikiri tunaishi enzi za gazeti la Uhuru na Mzalendo? Wanaishi nchi gani?
Kuhoji maamuzi na matendo ya viongozi wetu ni moja ya jukumu kubwa tulilonalo kama raia na wapiga kura. Ni haki na wajibu wa kila raia kuhoji kila linalofanywa na watumishi wetu.
Tutahoji maana tunataka kujua nani anasema ukweli kati ya serikali na Zitto.