VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, September 05, 2007
OKOA DUNIA KIJANA!

Mara nyingi nimekuwa nikipokea barua pepe kutoka kwa vijana wakiniuliza wafanye nini ili kusaidia au kuikoa dunia yetu. Huwa napata moyo sana ninapopokea barua pepe za namna hii.

Sasa naomba niseme kabisa kwamba ni wazi hakuna formula moja ya kusaidia dunia. Zipo njia mbalimbali, nyingi kuliko tunavyotizamia. Yapo mashirika yasiyo ya kiserikali chungu mbovu. Mengi kati ya hayo ni ya ukweli. Ni muhimu tukakumbushana kwamba yapo pia mengi tu ya uongo, yale yaliyo kwenye mikoba na matumbo ya wachache. Nchi za Afrika zinaongoza kwa kuwa na mashirikia ya namna hii. Serikali fadhili za magharibi ziliposema serikali za nchi nyingi za Afrika zimejaa ufisadi na hivyo wanaona ni bora wakawa wanatoa misaada yao kwa mashirika yasiyo ya kiserikali hawakujua kwamba viongozi wale wale wa serikali ndio pia wamiliki wa mashirika hayo. Ikawa ni pata potea.Halafu wazungu eti wanasema waafrika hatuna akili! Inakuingia akilini kweli. Sema tu ujanja wetu unakuwa hauna dira.Yaani unaiba hela, unanenepesha tumbo wakati ndugu na jamii yako inaangamia kwa sababu wewe ule mshiko wa kujengea dispensary umeenda kufaidi na hawara yako kwenye ile baa ya kona, pale mkwajuni , karibu na matuta mapya. Ama kweli.

Katika kujaribu kuangalia ni mashirika gani ambayo nadhani vijana wanaweza kujiunga nayo na kusaidia kuokoa dunia ni haya yafuatayo;

The Freechild Project

Free The Children

i-EARN

Peace Child International

TakingITGlobal

Youth Link


Zitembelee tovuti hizo na uangalie ni shirika lipi unadhani unaweza kushirikiana nalo katika harakati zako, iwe ni hapo mtaani kwako, mji unaoishi, wilaya, mkoa nk. Ukihitaji msaada wa tafsiri ya lugha ya kiingereza usisite kuwasiliana nami.

 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:40 PM | Permalink |


Maoni: 1


  • Tarehe: 5:37:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Poa kwa kunyooshea vidole harakati hizi zinazofaa vijana. Kuna ambazo nilikuwa nazijua ila nyingine ndio nimezijulia hapa.

    Halafu pale juu kuhusu mrembo yule kuwa kama rais wake. Ni jambo la kuchekesha ila kuna ukweli. Wewe kama una rais wa nchi inayoongea kiingereza lakini akawa hajui hicho kiingereza sawasawa...malizia.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker