VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Saturday, October 20, 2007
LAZIMA TUWE NA DEMOKRASIA?
Swali lililopo kwenye kichwa cha habari hapo juu linaweza kuwa rahisi sana usipofikiria kwa makini. Jibu la haraka haraka ni ndio, demokrasia ni lazima,ndio ubinadamu na utu kama sio kwenda na wakati.

Pamoja na hayo demokrasia bado ni mjadala mpana sana kwa sababu kila mtu anaweza akawa na maana yake na sote tukadai kuwa sawa na mwalimu akatuwekea ile alama ya vyema huku ikiwa na kimkato kidogo. Lakini je demokrasia ni suala la lazima?Sisi kama wananchi,walimwengu,binadamu wa karne hii ya 21 tunahitaji demokrasia? Na je, ungepewa nafasi ya kumchagua raisi wa dunia ungemchagua nani? Ni kweli kwamba wanawake ni mabingwa wa demokrasia kuliko wanaume? Ili kujibu maswali hayo na mengineyo mengi kuhusiana na suala zima la demokrasia,vijana fulani kutoka Afrika Kusini wameanzisha mjadala mkubwa kabisa mtandaoni kuwahi kutokea kuhusu suala hili. Tembelea tovuti ya Why Democracy?ujiunge katika mjadala, tizama documentaries, na kupanua mtazamo wako kuhusu demokrasia. Bonyeza hapa.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 3:02 PM | Permalink | Maoni 5
Friday, October 19, 2007
BARUA KWA MKAPA

Joseph Butiku-Hali ni mbaya

Utaratibu wa kuandikiana barua una historia ndefu sana.Mimi binafsi ni mmojawapo kati ya watu ambao hupenda kuandika barua.Iwe ni kwa kutakiana kheri, kuonyana au kukumbushana mambo fulani fulani. Nadhani, kwa mtazamo wangu,barua bado zitabakia kuwa msingi mzuri wa kubadilishana mawazo, ya shari au kheri. Siku hizi kilichobadilika ni jinsi barua inavyoandikwa.Badala ya kutumia mkono siku hizi tunatumia kompyuta.Bila kutumia posta siku hizi tunazituma kama barua pepe ingawa mimi bado naandikiana na babu na bibi zangu hizi hizi barua za kwenda posta na kuchungulia kale katundu.Ukikuta pamejaa vumbi tu unajua hamna kitu.

Jambo moja ambalo ninaamini ni kwamba, unapoandika barua (hususani baada ya kupima ujumbe unaotaka kuuandika) unakuwa umeketi chini na kujiuliza mara mia kidogo kuhusu barua yako. Je atakayeisoma ataielewa?Ataifanyia kazi?Ataichukuliaje na mambo kama hayo. Unaweza kukurupuka kuandika barua ya mapenzi au hata talaka.Ni jambo gumu kukurupuka kuandika barua yenye mstakabali wa nchi huku ukijua kabisa ule msemo wa wazungu usemao "a pen is a mighty sword". Niliwahi kuandika barua moja hivi kisha nikajuta.Bahati nzuri niliweza kuitetea kwa sababu nilichokuwa nimekiandika kilikuwa ni kweli na kinabakia kuwa kweli mpaka leo.Bado naamini hivyo kama vile Mwalimu Nyerere alivyoliamini Azimio la Arusha mpaka mauti ilipomkuta miaka nane iliyopita.


Ni kwa kuzingatia hayo hapo juu nimeisoma barua ya Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku(pichani) aliyomuandikia raisi wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa na kujishtukia naishiwa na pumzi. Utawezaje kuendelea kupumua katika mazingira yale?Sitaki kutoa hukumu ya moja kwa moja lakini wa kuangalia mazingira na hali halisi na pia kupima fikra za aliyeandika na aliyeandikiwa, nasema tena naishiwa pumzi.Hivi ni kweli hali ni mbaya kiasi hiki? Nikisema wapi tunaelekea nitakuwa naongopa.Swali sasa ni tumefikaje hapa na tufanye nini kuondoka? Soma barua hiyo hapa.


 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 1:28 PM | Permalink | Maoni 2
Thursday, October 04, 2007
UNA FURAHA?

Maisha bila furaha si maisha. Katika nchi zilizoendelea watu wengi sana hawana furaha wala raha ya maisha yao ukilinganisha na wale waliopo katika nchi zinazoendelea. Ndio maana inasemekana taifa lililo na furaha kupita yote duniani ni Nigeria ikifuatiwa na Mexico, Venezuela (hawa nasikia ndio wenye wanawake warembo kupita wote duniani) na El Salvador. Najua kama ulikuwa hujui hili unashangaa kwani ulidhani taifa hilo pengine lingekuwa ni Canada, Marekani au Uingereza. Maisha ya ughaibuni yamejaa presha. Ingia ndani ya gari lako au ndani ya basi kama sio treni saa za asubuhi kisha utizame sura ya jirani yako ndani ya basi au kwenye mataa uone kama anaonekana kuwa na furaha yoyote ya maisha. Utashangaa.

Watu wengi wanafanya kazi ambazo hawazipendi.Wamo kwenye mahusiano ambayo hayakidhi haja zao wala achilia mbali kukaribia japo robo ya ndoto zao. Msongo wa maisha umewajaa mpaka utosini. Idadi ya watu wanaojiua ni kubwa katika nchi zilizoendelea kuliko zinazoendelea au hata zile zilizogoma kuendelea!

Yawezekana wewe msomaji wangu huna furaha au tuseme raha ya maisha yako.Unaperuzi mtandaoni hivi leo ili tu kupunguza msongo wa maisha. Sasa ufanyeje ili kuwa na furaha au kufurahia maisha? Hebu jaribu kufanya yafuatayo;

  • Fanya mazoezi angalau kwa nusu saa tu mara tatu kwa wiki.
  • Hesabu Baraka zako. Siku inapofikia ukingoni jaribu kujiuliza ni mangapi ambayo wewe umebarikiwa kuwa nayo ambayo wengi hawana.

  • Tafuta muda wa maongezi- Jitahidi kupata muda wa kuketi chini na rafiki yako wa karibu au mpenzi wako mkaongea kwa uhuru na kinagaubaga.

  • Panda mti au ua na kisha lipalilie.

  • Tabasamu kwa mgeni utakayekutana naye leo.

  • Cheka-cheka kwa nguvu zako zote kila upatapo fursa.

  • Tenda jambo moja jema kwa siku.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:23 PM | Permalink | Maoni 7
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker