VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Friday, February 08, 2008
HII NDIO BONGO BWANA!

Leo siwezi tena kuomba msamaha kwa kutokuandika hapa mara kwa mara.Kama mnataka na mimi nijiuzulu kama waheshimiwa huko Tanzania….we acha tu.Vyeo vitamu bwana…si mlisikia wenyewe jinsi sauti za waheshimiwa zilivyokuwa zikitetemeka na kujaa mwangwi wakati wakitangaza kujiuzulu? Si mliona pia jinsi wengine hadi wake zao walivyoangua chozi?Unafanya mchezo nini? Hapo mimi ndipo ninaposhangaa,kama cheo au ukubwa unaupenda hivyo,kwanini usiwe mwadilifu basi?Eti kwanini? Kama wewe unajua kwamba hapa duniani unapenda kubebewa briefcase,unapenda kufunguliwa mlango wa gari na wa nyumba,unapenda kufungwa mkanda kama vile mtu uliye hoi kitandani,kwanini unaleta uzushi na uzabinabina unapokuwa madarakani?

Okei,sasa jamaa wametangaza kujiuzulu,mkuu wa nchi kakubali maombi yao..what next? Next ni kwamba jamaa bado wapo bungeni,tena bado wanachangia mijadala.Hii ndio bongo bwana.Changa la macho kama kazi. Hivi si ni ajabu kwamba unapojiuzulu,baada ya kukumbwa na kashfa nzito kama ya ufisadi,ubunge nao unatakiwa ukome mara moja? Mpiga kura gani anataka kuendelea kuwakilishwa na “fisadi’. Halafu Tanzania hamna hata ile sheria ya kuweza kum-recall mbunge.Yaani mkishamchagua,mnalo kwa miaka mitano.Linakuwa tsunami lenu tena. Halafu huko bungeni aliyemwaga manyanga jana leo anachangia na kusema Rais amechagua “mtu kama mimi”.Yaani wazi wazi kabisa mtu anasema,mmeuvaa tena mkenge.Na anapigiwa makofi na virungu! Ee bwana ndio…hii ndio bongo…kila mtu inabidi ajifanye hamnazo ili angalau kesho aweze kuamka na kwenda kazini. Hebu kwanza cheki hapo kama umeme upo bado au ushakata na kompyuta yako inatumia ule wa kudandia tu unaposoma habari hii.

Haya sasa,PM mwingine huyooo..anajinadi..anasema yeye ni mtoto wa kwanza(hata sijui hii inahusiana na nini).Anasema yeye ni mtoto wa mkulima.Alikuwa au bado ni mtoto wa mkulima? Kiswahili lazima tukitanue wajameni.Ahaaa…kumbe huyu naye anatoka pale pale…yaaani pale pale kwenye ofisi ya waziri mkuu! Halafu sura ni miongoni mwa zile zile.Bila woga na yeye anasema kumbe keshakaa sana pale ikulu..yaani anapajua kuliko hata nani sijui. Sasa hapo ndipo utakapochoka…kumbe sasa nini kipya hapa? Hapo hujazingatia jinsi mambo yalivyokwenda fasta? Hivi unataka kuniambia mambo yote haya,kimstakabali wa nchi..nasema nchi sio kijiji,yanafanyika ndani ya masaa kama 16 tu?? Kama ni kweli basi nchi yetu inastahili medani ya hali ya juu sana kwenye suala zima la disasters preparedness.

Wale wanaoitwa wapinzani…masikini hawa nao naona wamepigwa ganzi kiaina.Yaaani hata kuguna hawakuguna! Ingekuwa mimi ningesema haya ninayoyasema hapa.Eti nini…anaitwa nani?Pinda? Ofisi ya nani..Waziri Mkuu?

Sasa subiri baraza jipya la mawa-siri.Hapo ndipo utaweza kuthibitisha hizi hoja zangu.Kama unabisha tizama kama yule jamaa mwenye jina linalohusiana na vita vya majimaji hatarudi tena kwenye “kebineti”.Ni kama vile hakuna watu wengine wanaoweza kuwa mawaziri na manaibu waziri.Utasikia tu.Tena nasikia ule msururu wa mawaziri unarudi tena,tena na zaidi.Hii ndio bongo.

Aisee ukiona kimya sana hapa usidhani nimetoweka duniani..huwa pia naandika pale http://bongocelebrity.com.

 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:39 PM | Permalink |


Maoni: 8


  • Tarehe: 3:07:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Rama Msangi

    Jamani nimeuliza kuwa Ndesanjo kakumbwa na nini? Maana hata blogi yake siipati mimi, hebu nisaidieni wajameni

     
  • Tarehe: 6:03:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger EDWIN NDAKI (EDO)

    Jeff..nimependa sana tafakuri jadidi.

    Kweli hiyo ndio bongo mkuu.

    Na hao waliotemwa uwaziri usishangae sasa hivi ndio mabalozi watarajiwa.

    Mzee wa Rich/monduli naye bado anaitwa mh.Hakuna wa kumburuza popote.

    Ila poa tu..tutafika tu

     
  • Tarehe: 6:13:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger EDWIN NDAKI (EDO)

    Kweli nguvu zoote umeamishia BC..ila usitupe chungu cha zamani ..aaa aa


    ila Bc naikubali pia ipo tight.

    siku njema tutafika tu

     
  • Tarehe: 12:07:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Mzee Jeff,kama mmoja wa wadau wa JUMUWATA,wengi wangependa kusoma taarifa fupi ya maendeleo ya JUMUWATA.

    AMANI.

    RASTA HAPA.

     
  • Tarehe: 7:05:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous alat bantu sex

    thank you sir for the news you give this. really very good indeed. and I want to add a little bit of information specifically for adult men and women.

     
  • Tarehe: 7:06:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous vimax herbal

    I want to add a little bit of information specifically

     
  • Tarehe: 4:37:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger poker

    PROMO DELIMA
    poker online | Agen Domino | Agen Poker|Kumpulan Poker | bandar poker | Judi Poker | bandar qiu | Judi online terpercaya

    Bonus yang kami sediakan :
    * TO (Turn over) sebesar 0.3% yang akan di kami bagikan setiap hari senin
    * Bonus referal sebesar 10%

    Ayo segera daftarkan diri anda dan bergabunglah bersama kami !!
    Delimapoker.com Situs Agen Poker Online Terpercaya di Indonesia akan melayani Anda dengan profesional, memproses depo/wd dgn cepat.
    Come join and be a winer with us !!

    Untuk info selanjutnya silakan chat ke :
    Livechat_____: delimapoker
    BBM__________: 7B960959
    Facebook_____: Facebook
    Phone number_: +85595678845
    pendaftaran___http://www.delimapoker.com/?ref=19860605

     
  • Tarehe: 4:08:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger myslot

    ชอบหนังออนไลน์ต้องดู หนังใหม่ Alita: Battle Angel อลิตา แบทเทิล แองเจิ้ล (2019) สนุกดูฟรี

    https://www.doonung1234.com/

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker