VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Saturday, October 14, 2006
TUNAPOMKUMBUKA NYERERE!
(Picha kwa niaba ya Issa Michuzi)

Kama mtanzania, leo sina budi kuungana na watanzania wenzangu duniani kote kuadhimisha miaka 7 tangu Mwalimu J.K.Nyerere aage dunia kule Uingereza. Nafanya hivi kwa heshima niliyonayo juu ya kiongozi huyu aliyeongoza mapambano dhidi ya ukoloni na ukombozi wa bara zima la Afrika. Kinachomtofautisha Nyerere na viongozi wengine ni nia safi, imani halisi katika ukombozi wa muafrika.

Kinachotakiwa kufanyika hivi leo ni tafakuri za dhati juu ya uongozi wa Mwalimu,nini alikisimamia,nini alikiamini na kwa namna gani alifanikiwa au alishindwa. Tafakuri za namna hii sio tu zitatusaidia kujua historia bali kupanga vizuri mikakati ya taifa letu. Hatuwezi kuepuka kirahisi (pengine hatuna hata sababu) misingi waliyotuwekea Mwalimu na viongozi wenzake wa wakati ule. Mwalimu alijaribu. Kama binadamu yoyote yapo aliyokosea.Mimi nimemsamehe kwa sababu aliposhindwa alikiri, japo inawezekana kwamba alichelewa kukiri au kukubali kwamba amechemsha.

Kwa bahati mbaya siku hii ya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere imetekwa nyara ya wakora wa siasa. Leo hii utasikia hotuba chungu mbovu,utasikia neno "tumuenzi" kuliko neno lingine lolote. Hili hutia hasira kupita kiasi.Ukitaka kujua kiwango cha unafiki miongoni mwa viongozi wetu basi nenda tu viwanjani,majukwaani nk ukasikilize hotuba za viongozi katika maadhimisho haya. Naamini kabisa kwamba endapo viongozi wetu wangeitumia siku hii kujifanyia personal analysis ya uongozi wao basi "nchi ya ahadi" haingekuwa mbali kama ilivyo sasa.

Katika maadhimisho haya mwaka jana
niliandika namna hii (usisahau kusoma maoni ya wachangiaji). Ningeweza kabisa kuiweka makala ile kama ilivyo kwa sababu hakijabadilika kitu. Pengine swali ambalo sote tunabidi tujiulize ni unafiki umepungua au umeongezeka? Jibu sahihi unalo wewe msomaji. Hivi unadhani Nyerere angekuwa hai na kiongozi wa nchi angeweza kutokea Cuba kwenye mkutano wa nchi zisizofungamana na upande wowote na kisha kukimbilia Washington kupiga stori na "mkuu wa mabepari"? Unapoongelea kumuenzi Mwalimu unakuwa unamaanisha moja au mbili?

Tupende, tusipende jina la Nyerere limebakia kuwa nembo ya kisiasa tu.Viongozi wetu wa sasa wameamua,kwa makusudi, kulizika jina lake kwa "kutomuenzi" kama ahadi zao za kisiasa zinavyosema kila siku. Wanaolia na kumkumbuka kwa dhati ni wananchi wa kawaida ambao nao wanafanya hivyo kwa imani tu kwamba huenda angekuwa hai hili na lile lisingekuwa kama lilivyo hivi sasa. Huenda angeshazidiwa nguvu na majangili. Dalili za kuzidiwa nguvu zilianza kuonekana tangu akiwa hai. Unakumbuka msururu wa watu waliotaka kwenda ikulu mwaka 1995? Unajua wako wapi aliowakemea? Unajua mali wasizoweza kuzitolea hesabu zimeongezeka au zimepungua? Sasa nani anakudanganya kwamba kuna falsafa ya Mwalimu iliyobakia?


Yana mwisho haya.Tafakari.

 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 9:03 AM | Permalink |


Maoni: 4


  • Tarehe: 3:50:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Sultan Tamba

    Hapana shaka kwamba hakuna falsafa ya Mwalimu inayofuatwa, ni blabla tu, wakubwa wanaona aibu kuhusu siku hii, ila hawana jinsi, maana isipoadhimishwa itakuwa aibu kubwa zaidi. Lakini ukweli falsafa za mwalimu zimezikwa pamoja naye! Nikiangalia utawala mpya ulivyoanza, nina wasiwasi kwamba matabaka yataongezeka kuliko wakati mwingine wowote ule! Sasa hivi Rais na serikali yake wanakumbatia matajiri wa ndani na nje! Mifano iko mingi. Muda si muda, pengine haitazidi miaka mitano, masikini atakuwa hana chake tena katika nchi hii! Na hii italeta matatizo makubwa sana. Sasa hivi serikali inamwandama masikini katika namna ambayo ni dhahiri. Kwa mfano angalia sakata la wamachinga, wamefukuzwa kutoka katikati ya jiji wameelekezwa waende sehemu inaitwa Kigogo Sambusa, Mchikichini na huku relini nyuma ya stendi ya mabasi ya Scandinavia!
    Hapo Kigogo Sambusa ninapopita (maana mimi nakaa Magomeni kwa hiyo karibu kila siku hupita hapo), naona wamachinga wamejijengea wenyewe vibanda vya mbao tena bila mpangilio wowote, mbaya zaidi hili ni eneo la mkondo wa mto Msimbazi, ikija mvua biashara zote pale zitakufa maana Bahari huwa inahamia pale! Hata hivyo tangu vimejengwa hivyo vibanda hadi leo inakaribia mwezi, lakini hakuna hata mfanyabiashara mmoja aliyeanza kuuza! Hawapataki na kwa kweli hapafai! Wote wamekimbilia Mchikichini! Na sasa Mchikichini kumefurika! Umati uliojazana hapo, anajua Mungu na Mitume Yake! Mpaka barabara ya Uhuru inakaribia kutopitika!
    Kwa upande wa huku Relini, serikali imekwenda kuwavunjia tena, wanadai kwamba hawastahili kuwepo hapo na walipelekwa kwa makosa!
    Achilia mbali tatizo la Umeme!!
    Yaani ukiangalia masikini hawa wameshatupwa! Hakuna sera za Mwalimu zinazofuatwa. Na naamini mwalimu akifufuka leo halafu ajionee mwenyewe kilichoendelea baada ya yeye kufa, atakufa tena kwa mshtuko!

     
  • Tarehe: 12:20:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Mjengwa

    Jeff!
    Nimekusoma. Yote hayo yanatutaka tufikiri kwa bidii. Ama hakika ninachokiona sasa huku nyumbani ni ukweli kuwa umaarufu wa Mwalimu ni unazidi kuongezeka pengine kuliko alivyokuwa hai.

     
  • Tarehe: 2:59:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger afrikaoye

    This comment has been removed by a blog administrator.

     
  • Tarehe: 12:43:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    jeff

    shukurani kwa mawazo yako. mwalimu. mara nyingi napomfikiria baba haambiliki humuweka juu hata zaidi ya mandela kwa sana tu. (kumzungumzia mwalimu kijuu juu si rahisi. hasa kwa wenye busara na wanaoelewa na kutazama dunia ya leo kwa mtazamo wa marefu na mapana zaidi ya mipaka ya bongo au afrika mashariki au bara la afrika tu.) nasema au kumtaja au kumfananisha na modibo kwa sababu katika viongozi wa afrika huyu mzee ushujaa wake na sifa zake ndiyo zimetanda zaidi, lakini ni wa kihollywood (kwa maana ya kwamba wamarekani, waingereza na wazungu wengine ndiyo walioujenga ubingwa wake kwa kutumia vyombo kama vile tv magazeti na kadhalika kama hizo - bila kusahau waafrika wengi tu waliojitoa muhanga).

    tofauti ni kwamba mwalimu sifa zake ni za vitendo, huku akipigwa vita sana, nje na ndani ya nchi. kuna mmoja wetu anayeweza kumtaja kiongozi wa kiafrika mwenye sifa kama za huyu mzee marehemu (zaidi ya nkurumah, sankara na akina sobukwe, biko na huyo mandela, sidhani)? nikisema sifa nina maana sifa anazopewa na viongozi wenzake kwenye majukwaa ya kisiasa ulimwenguni. kwa mfano hotuba na mawazo yake yametafsiriwa kwa lugha tofauti na kuandikwa kama vitabu na yanafundishwa vyuo vikuu vilivyotapakaa ulimwenguni.

    kikwete na wakapa wengine hao hata kujulikana hawajulikani, achilia mbali kutajwa sehemu zinazoeleweka. hakuna, na sidhani kama hata mmoja wao aliyeishatoa mawazo au kuzungumzia kitu ambacho kimeonekana ni original kwenye ulingo wa kisiasa na ubunifu wenye manufaa, wenye kuleta msisimko au kuendeleza jamii ya kilimwengu – k.m. senghor na falsafa ya negritude - uafrika.

    ni kweli kabisa, na hapa humuweka mwalimu na kina malcom x (au alhaj malik shabaaz), mtu ambaye alijikuta akiimba sifa kwa watu wengine na kuhubiri mambo ya chuki, ambayo yalikubaliwa na wengi, lakini badala ya kuendelea kupiga mbiu ambayo ilikuwa ikisambaza makosa na kisirani, alikiri na kukubali kuwa alifanya mambo fulani kimakosa. hata kama alichelewa, ukweli unabaki kwamba alikiri na kukubali kuwa alikosea. si kitu rahisi. inataka mwanaume au shujaa haswa, awe mwanaume au mwanamke. viongozi wangapi wameona bora kwenda vitani na kuuwa maelfu, kama si mamilioni, ya watu kuliko kukiri makosa na kujitia kasoro.

    muhimu zaidi, undugu na umoja; kuwasisitizia wabongo juu ya lugha ya kuwaunganisha; jitihada zake kumfanya kila mtu angalau ajue kusoma na kuandika; kupunguza uhasama tokana na matabaka, udini, nk, ni baadhi tu ya vitu ambavyo malimu alicheza kama pele kwa manufaa ya wabongo wote.

    Tatizo: hata uwe mtu mbunifu na mwelevu vipi, iwapo itabidi kufanya kazi na watu wengine, au kwa kushihirikiana, wakikuachia ubebe kapu peke yako, hata kwa madawa huwezi kufaulu. pengine hao hao unaotakiwa kufanya nao kazi ndiyo wanaokuangusha kwa sababu zao binafsi. nkrumah yalimkuta, na sankara pia. na wote hawa ukiwaangalia utaona ni viongozi waliokuwa na mtazamo wa mapana na marefu, ukifananisha na kiongozi wa wastani afrika (ammbao wengi wanataka tu kujaza njuluku mifukoni mwao na kujiwekea sifa, au tuseme, kwa kifupi, wezi tu, fikiria . . . mobutu). waliangalia matatizo ya nchi zao kama matatizo ya afrika na kuelewa kuwa matatizo yanayowakabili waburkinabe, waghana, amaazania nk, ndiyo yale yale yanayowakabili wabongo, wakenya na wengineo.

    Wakapa na wenzao ni wapambe tu ambao, kama kunguni au fisi, wanangoja simba awinde na kuua wao wale mzoga aliobakisha. hebu fikiria, kama ni kweli, raisi wa nchi kwenda nunu ndege wakati hospitali dawa hakuna. huduma zinapatikana kwa wenye hela tu. kweli hawa ni viongozi wakuwasifu? kama unakula nao meza mojabasi kuwasifu ni wajibu. au kama unamakusudio ya kuja kuwa kama wao, kwani wao ndiyo mfano wa pale unapotaka kufikia. vinginveyo utawaona kama vile wanaiyoyomeza nchi kwa sababu ya ubinafsi wao. wanaweka mbele zaidi utandawizi, ambao haujakusudia kumnufaisha mlalahoi kamwe. kwa maneno mengine wakiokuja baada ya mchonga meno waliuuza kisiwa kabla hata hajafa. swali,: hivi sasa wabongo wana uhuru kiasi gani ukifananisha na enzi za kaizari? demokrasia ni ya vitendo au maneno tu kwa nza kabisa watu wanajua maana ya demokrasia? kichaka ambaye anachukuliwa kuwa ndo mfano wa siasa hii ya kidemokrasia ameshindwa vibaya sana kuongoza kwa mfano. ndiyo wataweza hao vikwete, wenye tama kuliko fisi?

    kweli baadhi yetu tutamkumbuka baba. kwa sababu nzuri na kwa sababu potofu. Nina bahati sana kuwa makuzi yangu yalikuwa ya enzi zake. ni kweli kabisa. Mwalimi alikuwa binadamu kama wengine, na hatuwezi kumsifu tu bila kukukubali kuwa alifanya makosa, kulikuwa na mengi sana ambayo sikuyapenda, na kuona kuwa tulikuwa tumebanwa. lakini baada ya kubahatika kuzunguka zunguka hapa na pale, nimeijukuta niko mbele ya wengi sana kimawazo na kimtazamo na elimu ya fikra, kifalsafa na moyo wa kibinadamu. nimeelewa maana ya kuchangia umaskini na tofauti ya ubinafsi na jumuiya.

    mwalimu alikuwa mwalimu kweli.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker